Saturday, February 11, 2012

Dawa za ARVs zathibitika kuzuia maambukizi ya Virus Vya Ukimwi!!

Hii ni habari njema kwa watu wanaoishi na VVU na jamii kwa ujumla:

Matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanyika Afrika na sehemu zingine duniani zimethibitisha kuwa kuna uwezekano wa zaidi ya asilimia 96 kwa mtu anaeishi na Virus vya Ukimwi kutowaambukiza wapenzi wao endapo watatutumia Dawa za kupunguza makali ya VVU kwa usahihi. Tafiti hizo ambazo baadhi zililazimika kusitishwa kabla ya muda wake uliopangwa baada ya matokeo ya awali kuonyesha mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa kampuni ya Kimarekani ya Utengenezaji wa Dawa za Kupunguza makali ya VVU - (tenofovir na emtricitabine), Gilead Science, imekili kusitisha tafiti zake kabla muda uliotegemewa kumalizika baada ya matokeo ya awali kuonyesha mafanikio makubwa katika nchi za Kenya na Uganda.

Kampuni hiyo iliendesha tafiti hizo kwa kuangalia matumizi ya sasa ya ARV ikiwemo huduma ya Post Exposure Prophylaxis (PEP) ambayo hutumiwa kuzuia maambukizi ya VVU kwa wahudumu wa afya wakati wa utoaji wa kuwahudumia wagonjwa, ambpo mhusika hupewa dozi hiyo ndani ya saa 72 baada ya kupata VVU, na ile ya Mama mjamzito dhidi ya mtoto wake wakati wa kujifungua (PMTCT).

Jumla ya wapenzi 4758 walihusishwa katika utafiti wa PrEP (Matumizi ya ARVs kwa watu wasio na VVU - Kinga). Katika utafiti huu, wapenzi wawili (mmoja mwenye VVU na mwingine asiye na VVU) walihusishwa kwa kutumia dawa aina ya tenofovir na emtricitabine (TDF/FTC). Utafiti huu ulionyesha kuwa matumizi ya dawa hizi kwa kila siku unaweza kupunguza uwezekano wa kuambukizana kwa aslimia 95. Hakukuwa na dalili ya athari zozote kwa dawa zote wakati wa matumizi hayo. Pia utafiti kama huo ulifanywa chini ya Mtandao wa Utafiti dhidi ya VVU (HPTN), ambao uliwahusisha wapenzi (discordant couples 1750) kwa kipindi cha miezi 78 katika nchi za Afrika, Asia na Marekani. Utafiti huo nao ulikoma baada ya mwaka mmoja kutokana na matokeo kuonyesha mafanikio makubwa

Tafiti hizi pia zimeibua hoja mpya ya muda unaofaa kwa watu wenye VVU kuanzishia "dozi ya ARVs" baada ya nchi mbalimbali kutofautiana eneo hilo. Hadi sasa nchi nyingi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, zimekuwa zikitumia Muongozo wa WHO ambao unapendekeza watu wanaoishi na VVU waanzishiwe Dozi hizo wanapofikisha CD4 kuanzia 350 kuja chini. Hata hivyo nchi za Marekani na Ulaya zimekataa kutumia muongozo huo na badala yake huwaanzishia watu wao mara wanapogundulika kuambukizwa au wanapofikisha CD4 kuanzia 500 na kuendelea. Hii inasemekana kuwa inaweza kutoa majibu ya kuwepo kwa tofauti kubwa ya watu wanaoishi na VVU, Maambukizi mapya na hata vifo vingi katika nchi maskini hasa Kusini ya Jangwa la Sahara, Barani Afrika na zile zilizoendelea za Ulaya na Marekani.

PAMOJA NA YOTE, HADI SASA HAKUNA UTAFITI ULIOFANYWA JUU YA FAIDA NA HASARA YA KUWAANZISHA DAWA HIZO MAPEMA.



Imeandaliwa na;
Dotto Athumani
Producer/Report
Graduate School of Journalism
UC Berkeley.
California.


contact: mnyadi@berkeley.edu, +1 (510) 666 7345

Friday, February 3, 2012

TABASAMU penye dhiki...kulikoni picha ya kiofisi kuumbwa na TABASAMU...?!

Picha moja huwakilisha maneno zaidi ya elfu moja. Huweza kueleza hisia ya mtu na hata tabia kwa ujumla. Zipo aina mbalimbali za picha, na hupigwa kwa malengo tofauti. Mojawapo ni picha inayopigwa kwa lengo la matumizi ya kiofisi, mfano kitambulisho, Pasi ya Kusafiri na zinazofanana na hizo. Kwa leo nitaizungumzia "Portrait" ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete.

Kawaida, Rais aliye madarakani anapaswa kuwa na picha katika ofisi mbalimbali za umma na hata zile binafsi ikiwa ishara ya kumtambua kama kiongozi halali wa Nchi. Picha hii ni moja ya picha zinazotumika katika mchakato huo na ni rahisi kuikuta katika ofisi mbalimbali za Serikali na Binafsi. Tatizo langu na picha hii ni "TABASAMU" la Mhe. Rais. Nilitegemea picha hii ingeundwa na Sura isiyoonyesha hisia yoyote (Neutral expression) kwa kuwa zipo sehemu haiwezi kulandana na tafsiri yake. Kwa mfano, Hospitalini, polisi na sehemu zingine zisizohitaji kumuona Rais akitabasamu.

Saturday, January 28, 2012

Hang Up strategy!!

Your telephone is for your personal use and you are not obligated to talk to anyone. Hang up if the caller does not speak or if you feel uncomfortable. Ask for the caller's identity or affiliation. If the caller gives an improper response, hang up. If the caller asks. "Who is this?" or "what number have I reached?" don't answer. Instead ask, "Who are you trying to reach?" or "What number did you call?" If the call is not legitimate, they will probably end it. If the caller persists after you have made it clear that don't' want to talk to them, the simplest response is to hang up.



REMEMBER Don't speak if you don't want to. Don't give out any information, and don't respond to questions if you don't know the caller

Monday, January 23, 2012

Kwanini watu wengi hupenda kwenda kusoma nchi za Magharibi?


Elimu ni ufunguo wa maisha, kauli hii iliwahi kuwa maarufu miaka ya 70 hadi 90 (sina uhakika kama bado inaaminiwa tena) na iliwahi kutumika kama chachu ya kuhamasisha vuguvugu la elimu barani Africa. Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele ndivyo gharama za elimu zimeendelea kuongezeka mara dufu. Pamoja na ongezeko hilo bado watu wengi wamekuwa wakikimbilia vyuo vya nje ikiwemo ulaya na Marekani ingawa takwimu zinaonyesha kuwa gharama ni kubwa kwa zaidi ya mara kumi ya zile wanakotoka. Kwa mfano, gharama za kusoma mwaka mmoja ngazi ya shahada nchini Marekani inafika Pesa za kitanzania milioni 30, huku shahada hiyo hiyo hugharimu kiasi cha milioni 2 hadi 5 za kitanzania.

Uchunguzi unaonyesha kuwa kuna tofauti kubwa ya ubora wa elimu inayotolewa kati ya nchi zilizoendelea na zile za dunia ya tatu. Kwa mfano ni rahisi sana kwa mwanafunzi wa uandishi wa Tanzania kumaliza shahada yake bila kujua chumba cha habari au kushika kifaa husika, wakati mwanafunzi wa fani hiyo hiyo katika nchi zilizoendelea akamaliza akiwa ameshaajiriwa katika chombo cha habari au kuanzisha cha kwake. Hii imetajwa kuwa sababu kubwa inayochelewesha maendeleo barani Afrika kutokana na ukweli kuwa wataalam wengi wanakosa ubunifu na uwezo baada ya kujifunza nadharia katika miaka yao yote ya mafunzo.